Share to: share facebook share twitter share wa share telegram print page

Switbati

Mt. Switbati alivyochorwa.

Switbati (pia: Suitbert, Suidbert, Suitbertus, Swithbert, au Swidbert; Northumbria, Uingereza, 647 hivi – Kaiserswerth, karibu na Dusseldorf, Ujerumani, 1 Machi 713) alikuwa mmonaki Mbenedikto wa Uingereza aliyepata umaarufu kwa kwenda umisionari pamoja na Wilibrodi kati ya makabila ya Ulaya Kaskazini.

Baada ya kupewa daraja ya juu na Wilfrido, alifanya utume huo kama askofu hasa katika Frisia na Westfalia, kati ya Uholanzi na Ujerumani za leo[1].

Mwaka 700 hivi alianzisha monasteri alimofariki.

Anaheshimiwa tangu zamani kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

  • John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 76-77
  • Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 64
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
Kembali kehalaman sebelumnya