Share to: share facebook share twitter share wa share telegram print page

Kikusa cha Uprogramishaji cha Programu tumizi

Kikusa cha Uprogramishaji cha Programu tumizi (kwa Kiingereza: Application Programming Interface, ufupi: API) ni kikusa kinachowezesha programu mbili tofauti kubadilishana data bila kujalisha tofauti katika utekelezaji wa michakato ya data katika hizo programu mbili. Mfumo ulio na API, hubainisha jinsi data itakavyopokelewa. Sehemu ya kupokea data huwa wazi na sehemu ya kuchakata data huwa dhahania, ikiwa imefichwa kwa watumizi wasio na ruhusa[1].

Seva ya API hufichua aina ya data, viumbile na kadhia zitakazopokelewa. Mteja hutuma data ikiwa katika fomati inayohitajika na seva. Kwa mfano, benki linaweza kuwa na API ambayo inaruhusu wateja kutuma ombi la salio. Katika kikusa, linaweza kuhitaji kuwepo kwa namba ya akaunti, msimbo wa usalama na jina la kadhia (ambalo ni ombi la salio). Seva itachakata kwa undani, kisha itoe jibu katika fomati iliyobainiwa. Ni wajibu wa mteja kujua fomati ili aweze kutuma data inavyofaa na programisha programu yake iweze kupokea majibu yatakayotolewa na seva.

Marejeo

  1. Reddy, Martin (2011). API design for C++. Burlington, MA: Morgan Kaufmann. ISBN 978-0-12-385003-4.
Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Kembali kehalaman sebelumnya