Chile
Chile, rasmi Jamhuri ya Chile, ni nchi iliyopo magharibi mwa Amerika Kusini, ikinukia kwenye stripi nyembamba kati ya Milima ya Andes na Bahari ya Pasifiki. Ni nchi ya kusini zaidi duniani na iliyo karibu zaidi na Antarctica. Inao idadi ya watu milioni 17.5 (kulingana na sensa ya 2017) na eneo la kilomita za mraba 756,102. Inapakana na Peru upande wa kaskazini, Bolivia upande wa kaskazini mashariki, na Argentina upande wa mashariki, na inadhibiti visiwa kadhaa vya Pasifiki. Mji mkuu wake ni Santiago, na lugha rasmi ni Kihispania.
Chile inadai ya kuwa sehemu ya bara la Antaktika ni eneo lake. ![]() Mji mkuu ni Santiago, yaani Mtakatifu Yakobo. JiografiaChile ina urefu wa kilomita 4,200 kufuata pwani ya Pasifiki na milima ya Andes. Umbali huu ni kama kutoka Cape Town kwenda Dar es Salaam. Lakini upana wa wastani wa eneo lake ni kilomita 180 tu: sehemu nyembamba ya nchi ina upana wa kilomita 90, sehemu pana zaidi ina kilomita 240. Nje ya maeneo yenye uwanja mwembamba wa pwani, nchi yote ni ya milima na mabonde. Sehemu kubwa ya nchi ina safu mbili za milima:
Katikati ya safu hizo mbili kuna bonde la kati (Valle Central) lenye makazi ya idadi kubwa ya wananchi na ardhi yenye rutuba kwa kilimo. Kuelekea kusini kimo cha nchi hushuka hadi kufikia chini ya uwiano wa bahari. Milima ya safu ya pwani huonekana sasa kama visiwa. Kaskazini mwa nchi hakuna bonde kubwa la kati. Nchi inapanda juu kutoka mwambao wa bahari hadi kuwa tambarare yenye kimo cha mita 1,000 - 1,500 inayoendelea mpaka mwanzo wa safu ya Andes. MilimaAndes za Chile ni kati ya milima ya juu duniani: kuna vilele kadhaa juu ya mita 6,000.
Watu![]() Wakazi wengi (85%) wanaishi mijini. Utafiti juu ya DNA yao unaonyesha kwa asilimia 52% hivi ina asili ya Ulaya, 43% ni ya Kiindio na 5% ni kutoka Afrika. Kwa jumla, wengi wana mchanganyiko wa damu. Lugha rasmi na ya kawaida ni Kihispania. Upande wa dini, 66.6% ni Wakatoliki na 17% ni Waprotestanti. Asilimia 12.4 haina dini yoyote. Tazama piaViungo vya nje
|